anacheza soka ya
kulipwa Marekani, amejiunga rasmi na
`Mabingwa Watarajiwa’ wa Ligi Kuu
ya Tanzania Bara msimu
huu, Simba.
Habari
za kutoka ndani ya klabu hiyo ambazo zimeenea
zinasema kuwa, usajili wa
mchezaji huyo umefanikishwa
na mmoja wa wafadhili wa zamani wa klabu
hiyo,
Azim Dewji.
Dewji
mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia hilo, alikiri na
kusema kuwa,
aliombwa na uongozi wa Simba kufanikisha
usajili wa mchezaji huyo na
kwamba baada ya kufanikiwa
, ameshamkabidhi Nizar kwa uongozi wa klabu.
“Kama
Mwanasimba, nimetimiza wajibu wangu kama
nilivyokuwa nimeombwa na
uongozi. Nimeambiwa
ataungana na wenzake kuanza mazoezi wakati wowote
kuanzia Jumatatu (leo),” alisema na kuongeza kuwa,
mchezaji huyo wa
zamani wa Mtibwa Sugar na
Moro United atakuwa na nafasi ya kuanza
kuichezea
Simba katika michuano ya kimataifa mwaka huu endapo
itaingia
hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.
Baada
ya kuzing’oa ya Kiyovu ya Rwanda na Setif ya
Algeria, wiki hii Simba
itaishukia Al Ahly Shandy ya
Sudan na kama ikifanikiwa kuvuka kiunzi
hicho
, itaingia katika raundi nyingine itakayoamua timu
za kucheza Nane
Bora Afrika.
Habari
zaidi zinasema kuwa, Nizar leo
atakabidhiwa rasmi jezi atakayoitumia
akiwa
Simba. Atakabidhiwa jezi hiyo siku moja kabla ya
mchezo wa Ligi
Kuu dhidi ya Moro United
unaotarajiwa kuanza saa kumi alasiri.
Mmoja
wa viongozi wa Simba ambaye hata
hivyo hakuwa tayari kutajwa jina
akisema si
msemaji, alikiri kukamilika kwa taratibu za Nizar
kutua Simba
huku akiongeza kuwa, ataisaidia
klabu hiyo katika michuano ya ligi na
ile ya
kimataifa kuanzia msimu ujao.
“Ni
kweli, timu inazidi kuimarika. Kumpata staa
wa kimataifa kama Nizar ni
jambo la kujivunia,
tunashukuru kwa juhudi zilizofanyika na hatimaye
kumpata mchezaji huyu,” alisema.
Nizar
ambaye Juni 21 mwaka huu atatimiza
umri wa miaka 24, kabla ya kutua
Simba
aliichezea Philadelphia Union ya Ligi Kuu ya
Marekani aliyodumu
nayo kwa miezi mitatu tu
baada ya kujiunga nayo akitokea Vancouver
Whitecaps. Alikuwa Vancouver tangu Agosti
22, mwaka 2009 akitokea Moro
United.
Katika
soka ya ushindani, nyota huyo aliibuki
a timu ya taifa ya vijana chini
ya umri wa
miaka 17, Serengeti Boys mwaka 2004 na
baadaye akajiunga na
Mtibwa Sugar kabla ya
kutimkia Kuwait kuichezea Al Tadamon ya
huko msimu
wa 2007-2008. Kutoka Tadamon
alikwenda Lebanon na kuichezea Tadamon
Sour
ya huko na mwaka 2009 aliichezea Moro United.
No comments:
Post a Comment