Tuesday, April 24, 2012


Ligi Kuu ya Vodacom imeingia raundi ya 25 ambapo 
kesho (Aprili 25 mwaka huu) Oljoro JKT itaikaribisha
 Yanga kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
 Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha wakati JKT
 Ruvu itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye
 Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Raundi hiyo itakamilika kwa mechi nne; Aprili 28
 mwaka huu Coastal Union itakuwa mwenyeji wa
 Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani
 jijini Tanga huku Mtibwa Sugar ikiwa mgeni wa
 African Lyon kwenye Uwanja wa Chamazi.

Azam na Toto African zitacheza Chamazi,
 Aprili 30 mwaka huu wakati Mei 1 mwaka
 huu Villa Squad itaumana na
 Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi.

Ligi hiyo itafunga msimu wa 2011/2012,
 Mei 5 mwaka huu ambapo timu zote
 14 zitakuwa uwanjani.

Simba vs Yanga (Uwanja wa Taifa),
 Oljoro JKT vs Polisi Dodoma
 (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha)
 na Ruvu Shooting vs Villa Squad (Mabatini, Mlandizi).

Mechi nyingine zitakuwa kati ya
 Coastal Union vs Toto African (Mkwakwani, Tanga), 
African Lyon vs JKT Ruvu (Manungu,
Morogoro), Azam vs Kagera Sugar (Chamazi, Dar es Salaam)
 na Moro United vs Mtibwa Sugar (Jamhuri, Morogoro).

No comments:

Post a Comment