Tuesday, April 24, 2012

NIZAR ASHINDWA KUTAMBULISHWA RASMI

 

Mchezaji mpya wa mabingwa wa tarajiwa wa

 Tanzania Bara Simba SC, Nizar Khalfan

 hakuweza kutambulishwa katika mchezo

 wa leo kama ilivyotangazwa hapo awali.


Akizungumza baada ya ushindi wa goli 3-0 

walioupata leo, ofisa habari wa Simba Ezekiel

 Kamwaga alisema kuwa zoezi la utambulisho 

lilishindikana baada ya Nizar Khalfan 

kuuguliwa na mamaake, hivyo kushindwa

 kufika katika uwanja wa Taifa.


Kamwaga alisema kuwa watapanga siku nyingine

 ya kumtambulisha kiungo huyo anayesifika kwa

 kupiga mashuti ya mbali, baada ya kushindikana leo.


Nizar amesajiliwa Simba SC kwa

 ajili ya michezo ya 

kimataifa kama watatinga hatua ya nane bora

 ya kombe la shirikisho CAF, na michuano

 ya Kagame Cup inayotarajiwa kurindima 

kati ya mwezi wa 6 ama wa 7 na msimu ujao.

No comments:

Post a Comment