Tuesday, April 24, 2012


BINGWA wa kick Boxing. Japhet Kaseba amesaini

 mkataba wa

 kucheza na Bingwa wa dunia wa ndondi 

mkanda unaomilikiwa

 na IBC, Francis Cheka wa Morogoro

 katika uzani wa 

KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba

 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba

 huo Kaseba

 amesema anashukulu kupata

 mpambano huo na

 atahakikisha anaonesha uwezo

 wake wote

 katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa

 wa mapambano;

"Najua mabondia wa hapa bongo

 wananikwep

a sana kwa kuwa nimeshakuwa bingwa

 wa ngumi 

za mateke lakini awajui mimi ni 

bingwa katika

 mapigano yote," alisema Kaseba.

"Nitahakikisha naweka kambi

 ya kutosha

 na kukata

 ngebe za cheka ni mtoto mdogo

 sana katika

 masumbwi kwa kweli bingwa wa

 kweli n

i Rashidi Matumla ambaye ninamuheshimu

 mpaka

 sasa Cheka kanikimbia mda mrefu tu

 tangia

 tupambane 3 October 2009 ambapo

 alipewa 

ubingwa kwa kusingizia mshabiki 

wangu, alikuja

 kumtupa nje ya uwanja kazi yake yeye

 anarudiana

 na Mada Maugo kila siku lakini kwa sasa

 kakanyaga miwaya zamu yake imefika."

Nae Promota wa mpambano huo Kaike

 Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika

 Dar es salaam siku ya sabasaba utakuwa ni

 mpambano ambao aujawai kutokea kwa kuwa

 mabondia hao wanakubalika na mashabiki

 wa ndani na nje ya Nchi.

Mbali na mpambano huo pia kutakua na

 mapambano ya utangulizi na burudani 

mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae.

No comments:

Post a Comment