MAKUSANYOKATIKA MICHEZO YA VPLNA NGORONGORO
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limewateua waamuzi
wanne wa
Tanzania kuchezesha mechi ya marudiano ya 16
bora ya Kombe la
Shirikisho kati ya Black Leopards
ya Afrika Kusini na Warri Wolves ya
Nigeria itakayochezwa
nchini Afrika Kusini kati ya Mei 4, 5 na 6 mwaka
huu.
Waamuzi hao ni Waziri Sheha atakayepuliza filimbi
wakati wasaidizi wake
watakuwa John Kanyenye
na Erasmo Jesse. Mwamuzi wa akiba
(fourth
official) atakuwa Israel Mujuni.
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Aurelio
Mathias wa Msumbiji.
Mechi ya kwanza kati ya timu hizo itachezwa Jumapili
(Aprili 29 mwaka
huu) kwenye Uwanja wa
Warri City ulioko Jimbo la Delta nchini Nigeria
na
itachezeshwa na waamuzi kutoka Senegal wakati
Kamishna atakuwa
Inyangi Bokinda wa Jamhuri
ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
1,635 WASHUHUDIA MECHI YA YANGA, POLISI DODOMA
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Polisi
Dodoma iliyochezwa
(Aprili 22 mwaka huu)
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
ilishuhudiwa
na watazamaji 1,635 na kuingiza sh. 5,666,000.
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na
asilimia 18 ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT)
ambayo ni sh. 864,305.08 kila klabu ilipata
sh. 193,858.47, uwanja sh. 26,469.49. Shirikisho
la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) sh. 26,469.49,
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Dar es
Salaam (DRFA) sh. 108,687.80.
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu
(FDF) sh. 13,234.75, Baraza la Michezo la Taifa
(BMT) sh. 2,646.95 na
asilimia 10 ya gharama
za mechi ni sh. 26,469.49.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani
kwa waamuzi sh.
10,000, nauli ya ndani kwa
kamishna wa mchezo sh. 10,000. Mwamuzi wa
akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna
na waamuzi sh.
160,000, gharama ya tiketi sh. 1,500,000
, usafi na ulinzi kwa uwanja
sh. 1,500,000 na Wachina
(Beijing Construction) sh. 1,000,000.
Kutokana na mechi hiyo kuingiza kiasi kidogo baadhi ya
gharama
zililipwa nusu au kutolipwa kabisa na kuacha
madeni. Madeni hayo ni
tiketi sh. 1,500,000,
maandalizi ya uwanja (pitch marking) sh. 400,000,
umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja
sh. 850,000 na Wachina
sh. 1,000,000.
POLISI MORO, MGAMBO, PRISONS ZAPANDA VPL
Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) iliyoshirikisha
timu tisa
imemalizika jana (Aprili 23 mwaka huu)
kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro huku tatu zikifuzu kucheza Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa
2012/2013
utakaonza Agosti mwaka huu.
Timu hizo ni Polisi Morogoro iliyofikisha pointi
20 ikifuatiwa na
Mgambo Shooting ya
Tanga (15) na Tanzania Prisons ya Mbeya
iliyomaliza
katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 14.
Nyingine zilizofuatia na pointi zao kwenye
mabano ni Polisi Dar es
Salaam (13),
Mbeya City Council (11), Rhino Rangers ya Tabora (8),
Mlale JKT ya Ruvuma (8), Polisi Tabora (6) na
Transit Camp ya Dar es
Salaam (2).
SIMBA, MORO UNITED ZAINGIZA MIL 28/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na
Moro United
lililochezwa jana (Aprili 23 mwaka huu)
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
limeingiza sh. 28,688,000.
Jumla ya watazamaji 7,945 walikata tiketi kushuhudia
mechi hiyo kwa
viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000,
sh. 10,000 na sh. 15,000.
Watazamaji 6,946 kati ya
hao walishuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha
sh. 3,000.
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na
asilimia 18 ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT)
ambayo ni sh. 4,376,135.59 kila klabu
ilipata
sh. 4,919,009.32, uwanja sh. 1,454,286.44.
Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) sh.
1,454,286.44, Chama cha Mpira wa Miguu
Mkoa wa Dar
es Salaam (DRFA) sh. 1,058,414.58,
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu
(FDF)
sh. 727,143.22, Baraza la Michezo la Taifa (BMT)
sh. 145,428.64
na asilimia 10 ya gharama za
mechi ni sh. 1,454,286.44.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya
ndani kwa waamuzi sh.
10,000, nauli ya ndani
kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000, mwamuzi
wa
akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa
kamishna na waamuzi sh. 80,000,
gharama
ya tiketi sh. 3,000,000, maandalizi ya
uwanja (pitch) sh.
400,000, umeme sh. 300,000,
usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na
Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.
Nayo mechi kati ya Villa Squad na African Lyon
iliyochezwa Aprili 22
mwaka huu kwenye
Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam
iliingiza sh. 496,000
ambapo kila klabu ilipata
sh. 68,061.70 wakati watazamaji
walioshuhudia
mechi hiyo ni 469.
Vilevile mechi kati ya
Tanzania (Ngorongoro Heroes) na
Sudan iliyochezwa Aprili 21 mwaka huu
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
iliingiza sh. 9,717,000 kutokana na
washabiki 2,562.
No comments:
Post a Comment