MNYAMA ATWAA UBINGWA
Wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa kwa
ngazi klabu, Simba SC wametwawazwa Ubingwa wa
Tanzania Bara baada ya Kushinda goli 3-0,
huku wapinzani wake katika mbio hizo Azam FC
wakitoka sare ya goli 1-1.
Katika mchezo huo wa ligi kuu ya vodacom
Simba SC waliandika goli la kwanza kupitia
kwa Patrick Mafisango, huku Haruna Moshi
Boban akiiandikia goli la pili.
Simba walihitimisha goli la 3 kupitia kwa
Felixs Sunzu, na mpaka kipenga cha mwisho
Simba SC 3-0 Moro united
Katika mchezo mwingine uliochezwa
Chamanzi kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar
ulivunjika baada ya Mtibwa Sugar walio kuwa
pungufu kugomea penati ya Azam FC katika
dakika za majeruhi.
Mchezo huo ulivunjika matokeo ya kiwa goli 1-1,
yaliyofungwa na Salum Swedi kwa upande wa
Mtibwa na Mrisho Ngassa kwa upande
wa Azam FC
No comments:
Post a Comment