Monday, April 23, 2012

MNYAMA ATWAA UBINGWA

Wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa kwa

ngazi klabu, Simba SC wametwawazwa Ubingwa wa

 Tanzania Bara baada ya Kushinda goli 3-0,

huku wapinzani wake katika mbio hizo Azam FC

wakitoka sare ya goli 1-1.

 Katika mchezo huo wa ligi kuu ya vodacom

 Simba SC waliandika goli la kwanza kupitia

 kwa Patrick Mafisango, huku Haruna Moshi

Boban akiiandikia goli la pili.

 Simba walihitimisha goli la 3 kupitia kwa

 Felixs Sunzu, na mpaka kipenga cha mwisho

Simba SC 3-0 Moro united

 Katika mchezo mwingine uliochezwa

Chamanzi kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar

 ulivunjika baada ya Mtibwa Sugar walio kuwa

pungufu kugomea penati ya Azam FC katika

 dakika za majeruhi.

 Mchezo huo ulivunjika matokeo ya kiwa goli 1-1,

yaliyofungwa na Salum Swedi kwa upande wa

Mtibwa na Mrisho Ngassa kwa upande

        wa Azam FC


No comments:

Post a Comment