Tuesday, April 24, 2012


Ligi Kuu ya Vodacom imeingia raundi ya 25 ambapo 
kesho (Aprili 25 mwaka huu) Oljoro JKT itaikaribisha
 Yanga kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
 Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha wakati JKT
 Ruvu itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye
 Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Raundi hiyo itakamilika kwa mechi nne; Aprili 28
 mwaka huu Coastal Union itakuwa mwenyeji wa
 Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani
 jijini Tanga huku Mtibwa Sugar ikiwa mgeni wa
 African Lyon kwenye Uwanja wa Chamazi.

Azam na Toto African zitacheza Chamazi,
 Aprili 30 mwaka huu wakati Mei 1 mwaka
 huu Villa Squad itaumana na
 Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi.

Ligi hiyo itafunga msimu wa 2011/2012,
 Mei 5 mwaka huu ambapo timu zote
 14 zitakuwa uwanjani.

Simba vs Yanga (Uwanja wa Taifa),
 Oljoro JKT vs Polisi Dodoma
 (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha)
 na Ruvu Shooting vs Villa Squad (Mabatini, Mlandizi).

Mechi nyingine zitakuwa kati ya
 Coastal Union vs Toto African (Mkwakwani, Tanga), 
African Lyon vs JKT Ruvu (Manungu,
Morogoro), Azam vs Kagera Sugar (Chamazi, Dar es Salaam)
 na Moro United vs Mtibwa Sugar (Jamhuri, Morogoro).

MAKUSANYOKATIKA MICHEZO YA VPLNA NGORONGORO

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limewateua waamuzi 

wanne wa Tanzania kuchezesha mechi ya marudiano ya 16

 bora ya Kombe la Shirikisho kati ya Black Leopards

 ya Afrika Kusini na Warri Wolves ya Nigeria itakayochezwa

 nchini Afrika Kusini kati ya Mei 4, 5 na 6 mwaka huu.


Waamuzi hao ni Waziri Sheha atakayepuliza filimbi

 wakati wasaidizi wake watakuwa John Kanyenye

 na Erasmo Jesse. Mwamuzi wa akiba

 (fourth official) atakuwa Israel Mujuni.

 Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Aurelio

 Mathias wa Msumbiji.


Mechi ya kwanza kati ya timu hizo itachezwa Jumapili

 (Aprili 29 mwaka huu) kwenye Uwanja wa

 Warri City ulioko Jimbo la Delta nchini Nigeria na

 itachezeshwa na waamuzi kutoka Senegal wakati

 Kamishna atakuwa Inyangi Bokinda wa Jamhuri

 ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).


1,635 WASHUHUDIA MECHI YA YANGA, POLISI DODOMA


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Polisi

 Dodoma iliyochezwa (Aprili 22 mwaka huu)

 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

 ilishuhudiwa

 na watazamaji 1,635 na kuingiza sh. 5,666,000.


Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na

 asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT)

 ambayo ni sh. 864,305.08 kila klabu ilipata

 sh. 193,858.47, uwanja sh. 26,469.49. Shirikisho

 la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 26,469.49, 

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa 

Dar es Salaam (DRFA) sh. 108,687.80.

 Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu

 (FDF) sh. 13,234.75, Baraza la Michezo la Taifa

 (BMT) sh. 2,646.95 na asilimia 10 ya gharama

 za mechi ni sh. 26,469.49.


Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani

 kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa

 kamishna wa mchezo sh. 10,000. Mwamuzi wa

 akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna

 na waamuzi sh. 160,000, gharama ya tiketi sh. 1,500,000

, usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 1,500,000 na Wachina

 (Beijing Construction) sh. 1,000,000.


Kutokana na mechi hiyo kuingiza kiasi kidogo baadhi ya

 gharama zililipwa nusu au kutolipwa kabisa na kuacha

 madeni. Madeni hayo ni tiketi sh. 1,500,000, 

maandalizi ya uwanja (pitch marking) sh. 400,000,

 umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja

 sh. 850,000 na Wachina sh. 1,000,000.


POLISI MORO, MGAMBO, PRISONS ZAPANDA VPL


Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) iliyoshirikisha

 timu tisa imemalizika jana (Aprili 23 mwaka huu)

 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini

 Morogoro huku tatu zikifuzu kucheza Ligi

 Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2012/2013

 utakaonza Agosti mwaka huu.


Timu hizo ni Polisi Morogoro iliyofikisha pointi 

20 ikifuatiwa na Mgambo Shooting ya

 Tanga (15) na Tanzania Prisons ya Mbeya

 iliyomaliza katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 14.


Nyingine zilizofuatia na pointi zao kwenye

 mabano ni Polisi Dar es Salaam (13),

 Mbeya City Council (11), Rhino Rangers ya Tabora (8),

 Mlale JKT ya Ruvuma (8), Polisi Tabora (6) na

 Transit Camp ya Dar es Salaam (2).


SIMBA, MORO UNITED ZAINGIZA MIL 28/-


Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na

 Moro United lililochezwa jana (Aprili 23 mwaka huu)

 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 28,688,000.


Jumla ya watazamaji 7,945 walikata tiketi kushuhudia

 mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000,

 sh. 10,000 na sh. 15,000. Watazamaji 6,946 kati ya

 hao walishuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000.


Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na

 asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT)

 ambayo ni sh. 4,376,135.59 kila klabu

 ilipata sh. 4,919,009.32, uwanja sh. 1,454,286.44.

 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh.

 1,454,286.44, Chama cha Mpira wa Miguu

 Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,058,414.58,

 Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF)

 sh. 727,143.22, Baraza la Michezo la Taifa (BMT)

 sh. 145,428.64

 na asilimia 10 ya gharama za 

mechi ni sh. 1,454,286.44.


Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya

 ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani

 kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000, mwamuzi

 wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa

 kamishna na waamuzi sh. 80,000, gharama

 ya tiketi sh. 3,000,000, maandalizi ya

 uwanja (pitch) sh. 400,000, umeme sh. 300,000,

 usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na

 Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.


Nayo mechi kati ya Villa Squad na African Lyon

 iliyochezwa Aprili 22 mwaka huu kwenye

 Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam 

iliingiza sh. 496,000 ambapo kila klabu ilipata

 sh. 68,061.70 wakati watazamaji

 walioshuhudia mechi hiyo ni 469.


Vilevile mechi kati ya

Tanzania (Ngorongoro Heroes) na

 Sudan iliyochezwa Aprili 21 mwaka huu

 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam 

iliingiza sh. 9,717,000 kutokana na

 washabiki 2,562.


BINGWA wa kick Boxing. Japhet Kaseba amesaini

 mkataba wa

 kucheza na Bingwa wa dunia wa ndondi 

mkanda unaomilikiwa

 na IBC, Francis Cheka wa Morogoro

 katika uzani wa 

KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba

 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba

 huo Kaseba

 amesema anashukulu kupata

 mpambano huo na

 atahakikisha anaonesha uwezo

 wake wote

 katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa

 wa mapambano;

"Najua mabondia wa hapa bongo

 wananikwep

a sana kwa kuwa nimeshakuwa bingwa

 wa ngumi 

za mateke lakini awajui mimi ni 

bingwa katika

 mapigano yote," alisema Kaseba.

"Nitahakikisha naweka kambi

 ya kutosha

 na kukata

 ngebe za cheka ni mtoto mdogo

 sana katika

 masumbwi kwa kweli bingwa wa

 kweli n

i Rashidi Matumla ambaye ninamuheshimu

 mpaka

 sasa Cheka kanikimbia mda mrefu tu

 tangia

 tupambane 3 October 2009 ambapo

 alipewa 

ubingwa kwa kusingizia mshabiki 

wangu, alikuja

 kumtupa nje ya uwanja kazi yake yeye

 anarudiana

 na Mada Maugo kila siku lakini kwa sasa

 kakanyaga miwaya zamu yake imefika."

Nae Promota wa mpambano huo Kaike

 Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika

 Dar es salaam siku ya sabasaba utakuwa ni

 mpambano ambao aujawai kutokea kwa kuwa

 mabondia hao wanakubalika na mashabiki

 wa ndani na nje ya Nchi.

Mbali na mpambano huo pia kutakua na

 mapambano ya utangulizi na burudani 

mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae.

NIZAR ASHINDWA KUTAMBULISHWA RASMI

 

Mchezaji mpya wa mabingwa wa tarajiwa wa

 Tanzania Bara Simba SC, Nizar Khalfan

 hakuweza kutambulishwa katika mchezo

 wa leo kama ilivyotangazwa hapo awali.


Akizungumza baada ya ushindi wa goli 3-0 

walioupata leo, ofisa habari wa Simba Ezekiel

 Kamwaga alisema kuwa zoezi la utambulisho 

lilishindikana baada ya Nizar Khalfan 

kuuguliwa na mamaake, hivyo kushindwa

 kufika katika uwanja wa Taifa.


Kamwaga alisema kuwa watapanga siku nyingine

 ya kumtambulisha kiungo huyo anayesifika kwa

 kupiga mashuti ya mbali, baada ya kushindikana leo.


Nizar amesajiliwa Simba SC kwa

 ajili ya michezo ya 

kimataifa kama watatinga hatua ya nane bora

 ya kombe la shirikisho CAF, na michuano

 ya Kagame Cup inayotarajiwa kurindima 

kati ya mwezi wa 6 ama wa 7 na msimu ujao.

Monday, April 23, 2012

ROBIN VAN PERSIE AN'GARA



Robin Van Persie atwaa tuzo ya mwanasoka bora wa kulipwaNaye beki
wa kulia wa Totenham Hotspurs Kyle Walker alichaguliwa mwanasoka
bora kijana akiwashinda Sergio Aguero na Danny Welbeck.

Premier League team of the year:

Joe Hart (Man City), Kyle Walker (Tottenham), Vincent Kompany (Man City),
Fabricio Coloccini (Newcastle), Leighton Baines (Everton)
, David Silva (Man City), Yaya Toure (Man City), Gareth Bale (Tottenham),
Scott Parker (Tottenham), Robin van Persie (Arsenal), Wayne Rooney (Man Utd).

Championship team:

Kelvin Davis (Southampton), Nathaniel Clyne (Crystal Palace)
, James Tomkins (West Ham), Curtis Davies (Birmingham),
Ian Harte (Reading), Adam Lallana (Southampton),
Peter Whittingham (Cardiff), Mark Noble (West Ham),
Matt Phillips (Blackpool), Rickie Lambert (Southampton), 
Jay Rodriguez (Burnley).

MNYAMA ATWAA UBINGWA

Wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa kwa

ngazi klabu, Simba SC wametwawazwa Ubingwa wa

 Tanzania Bara baada ya Kushinda goli 3-0,

huku wapinzani wake katika mbio hizo Azam FC

wakitoka sare ya goli 1-1.

 Katika mchezo huo wa ligi kuu ya vodacom

 Simba SC waliandika goli la kwanza kupitia

 kwa Patrick Mafisango, huku Haruna Moshi

Boban akiiandikia goli la pili.

 Simba walihitimisha goli la 3 kupitia kwa

 Felixs Sunzu, na mpaka kipenga cha mwisho

Simba SC 3-0 Moro united

 Katika mchezo mwingine uliochezwa

Chamanzi kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar

 ulivunjika baada ya Mtibwa Sugar walio kuwa

pungufu kugomea penati ya Azam FC katika

 dakika za majeruhi.

 Mchezo huo ulivunjika matokeo ya kiwa goli 1-1,

yaliyofungwa na Salum Swedi kwa upande wa

Mtibwa na Mrisho Ngassa kwa upande

        wa Azam FC


ZAWADI YA PAMBANO LA CHEKA NA MAUGO HADHARANI



 Johabes Lugenge kushoto na Lucas Rutainurwa   

WAANDAAJI wa pambano la ubingwa wa IBF kati ya Francis
Cheka na Mada Maugo leo wameonesha rasmi
 gariwatakalogombania  Mabondia
Mada Maugo Na Francis
Cheka  Aprili 28 mwaka huu katika ukumbi wa PTA,
Dar es Salaam.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa katika uzito wa
kg 75 la raundi 12 la Kimataifa ambapo linatarajiwa
kuwa chini ya Kamisheni ya Kamisheni ya Ngumi za
Kulipwa Tanzania (TPBC) huku majaji wa pambano
hilo wakitegemewa kutoka nje ya nchi.
Akizungumza Dar es Salaam leo, Msemaji wa
mpambano huo Yasini Abdallah amesema
kuanikwa kwa mkanda huo na Gari kuwekwa
Hadharani kutaashiria kupamba moto kwa pambano
hilo ambalo linatarajia kuwa katika ngazi ya Kimataifa
ili kuweza kupatikana kwa mshindi wa halali na pia litafuta
hisia za kuwepo na ubabaishaji katika pambano hilo.
kaike amesema kuwa wameamua kuanika
Gari na mkanda ili kuwathibitishia wadau wa
ngumi na mashabiki kwa ujumla kuwa wapo
 makini na pambano hilo na sio la kibabaishaji na
kama walivyosema hapo awali kuwa majaji watoka
nje ya nchi na hiyo yote ni kutaka mchezo uchezeshwe
kulingana na hadhi ya mkanda
Amesema, maandalizi kwa ujumla ya pambano
hilo yanaendelea vizuri na zawadi ya gari kwa
mshindi liko pale pale ambapo mshindi atakabidhiwa
siku hyio hyio ya pambanomra tu  baaday ya
kutangazwa mshindi na kupewa mkanda
itafuatiwa na zawadi hiyo ya gari.
Awali mabondia hao walishakutana mara
mbili ulingoni ambapo katika pambano la
kwanza lilofanika PTA Cheka alishinda kwa
pointi ambapo Maugo hakukubali matokeo
hao na kuandaliwa pambano la marudiano
lilofanyika Uwanja wa Jamuhuri Morogoro
ambapo Cheka aliibuka mshindi tena kwa
kumtwanga kwa pointi.
Baada ya kumalizika kwa pambano hilo kila
bondia aligoma kucheza na mwenzake tena
lakini baada ya kuandaliwa pambano hilo la
ubingwa kila mmoja alibadilisha nia na kuamua
kurudi ulingoni kuwania mkanda huo.